Headlines News :

Wednesday, October 2, 2013

CHOMBEZO : FACEBOOK CHATTIN' - 9



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
SIMU: 0718 069 269.
FACEBOOK CHATTING 9


Baba yake Aziza alikuwa amenitolea macho pamoja na wageni wote ambao walikuwa sebuleni, mtu mzima sikutaka kuteteleka hata kidogo, nilionyesha uso wa kujiamini kupita kawaida. Kwa Aziza, kwa mbali alionekana kuwa na hofu kwani alidhani kwamba nisingekuwa na ujasiri wa kusimama na kuzungumza.

MIMI: Samahani mzee. Shikamoo.
BABA AZIZA: Marahaba.
MIMI: Nilikuja katika kipindi kilichopita lakini sikukuta.
BABA YAKE AZIZA: Sikuwepo. Sawa, umeshanikuta. Kuna nini?
MIMI: Niliagizwa na mzee Badour wa kule Msasani, ameniambia kwamba leo utatakiwa kufika katika kikao kile cha harusi kinachoendelea (Baba Aziza akaonekana kushtuka)
BABA AZIZA: Kikao gani?
MIMI: Kile cha mtoto wake, Farhia.
BABA AZIZA: Huyo mzee ndiye nani?
MIMI: Mfanyabiashara mwenzako.
BABA AZIZA: (Huku akionekana kushangaa zaidi) Alikutuma uje kwangu?
MIMI: Ndio (Nilijibu huku nikiwa serious)
BABA AZIZA: Una uhakika ni mimi?
MIMI: Ndio.
BABA AZIZA: Yeye alikwambia uende kwa nani?
MIMI: Kwako.
BABA AZIZA: Nani?
MIMI: Mzee Mahmoud.
BABA AZIZA: Hapana. Mimi sio mzee Mahmoud. Mimi ni mzee Mansour.
MIMI: Mmmh! Mbona unanichanganya? Hii si nyumba namba 315?
BABA AZIZA: Hapana. Hii ni nyumba namba 511. Nyumba kuanzia namba 300 zipo kule mbele.
MIMI: Ok! Basi samahani kwa usumbufu mzee wangu. Nikosea namba, ila nilipomuuliza mlinzi alijibu hapa ni kwa mzee Mansour ila jina likanichanganya, si unajua sisi wengine majina ya kiarabu hatuyajui vizuri.
BABA AZIZA: Usijali kijana. Najua vijana wa sasa hivi mnakuwa na mambo mengi vichwani. Sawa. Nenda.
MIMI: Usijali (Nikageuka na kisha kuufungua mlango huku Aziza akibaki kutetemeka tu)
MLINZI: Ebwanaa vipi tena, mbona sikuelewi elewi?
MIMI: Hakuna tatizo. Nilikuwa nataka kuonana na mzee Mansour tu.
MLINZI: Ok! Karibu tena.
MIMI: Asante.

Nikashusha pumzi ndefu, sikuamini kama niliweza kutoka katika mikono ya mzee yule aliyeonekana kuwa na hasira kupita kawaida. Nilitembea kwa mwendo wa haraka haraka mpaka kituoni ambapo nikapanda gari na kisha kuelekea nyumbani. Garini, mawazo yangu yalikuwa juu ya ule msala ambao nilikuwa nimenusurika, ulikuwa msala mkubwa ambao ungeweza kunitoa roho kama ningeleta ishu za Kisharobaro kama Eduado. Nilipofika nyumbani, nikaanza kuchati na Aziza.

AZIZA: Hakuna kama wewe. Umeshindikana mpenzi. Wewe ni genius.
MIMI: Hahaha! Tena ana bahati leo sikutaka kuleta usanii mkubwa zaidi.
AZIZA: Mmh! Kwani ungeweza kuleta zaidi ya ule?
MIMI: Yeah! Mngenibeba pale.
AZIZAl: Hahaha! Hapana chezea wewe mtoto wa tandale, umeshindikana aisee.
MIMI: Hahaha! Usijali. Kokote kunapokuwa na ishu zinazohitaji mafunzo ya kininja wewe niite tu, usiogope. Hata ukitaka kuingia Ikulu, wewe niite tu na kila kitu kitakuwa poa.
AZIZA: Mmmh! Unajiamini wewe.
MIMI: Acha masihala na mimi.
AZIZA: Ok! Leo sichati sana ila ningependa kuonana na wewe kesho.
MIMI: Wapi?
AZIZA: Popote upendapo.
MIMI: Poa. Tuonane gesti.
AZIZA: Hahaha! Acha masihala.
MIMI: Ndio maana nimekwambia sema wapi. Yaani ni sawa na kuja Tandale halafu nikuulize unakunywa kinywaji gani, je ukisema maziwa, nitayatoa wapi? Ukija huku sikuulizi unakunywa kinywaji gani, nakuuliza unakunywa soda gani.
AZIZA: Hahah! Wewe mtoto wewe. Najivunia kuwa na mtu kama wewe.
MIMI: Usijali. Kuwa serious, tuonane wapi?
AZIZA: Njoo chuo.
MIMI: Saa ngapi?
AZIZA: Muda wowote ule.
MIMI: Poa. Nitakuja saa nne usiku.
AZIZA: Nini?
MIMI: Hebu kuwa serious, nije saa ngapi?
AZIZA: Njoo saa tisa. Unalijua lile jengo la Biashara la UDBS?
MIMI: Yeah! Si pale karibu na kituo cha polisi, opposite na mini-market?
AZIZA: Yeah!
MIMI: Poa nitakuja.
AZIZA: Usichelewe, kuna bonge la sapraizi nataka kukuonyeshea.
MIMI: Mmmh! Lipi hilo?
AZIZA: Nikikwambia haitokuwa sapraizi. Wewe njoo tu.
MIMI: Poa.

Kuanzia kipindi hicho sikuonekana kuwa na furaha tena, muda wote nilikuwa nafikiria kuhusiana na sapraizi hiyo ambayo Aziza alikuwa ameniahidi. Sikufichi rafiki yangu, usiku ulikuwa mrefu kwangu. Sikutaka kuchati na Aziza, nililala moja kwa moja mkpaka kesho ambapo nikaamka. Kutokana na ubize wa hapa na pale, nikaenda chuo saa tisa na kisha kumuita aje nje ya jengo lile la UDBS, haukuchukua muda, akatoka huku akiwa na Eduado, wote walikuwa wakicheka jambo lililonichanganya.

AZIZA: Karibu mpenzi.
MIMI: Asante. Mbona mnacheka hivyo mtafikiri mnamwangalia Mr Bean?
EDUADO: Ungekufa. Watoto wa Waarabu si wa kwenda kuwavaminia kwao. Matokeo yake ukajificha uvunguni, sikupatii picha, ulijikunja kama dawa ya mbu.
MIMI: Hahaha! Aisee ni noma. Kweli nimeamini mtu akifumaniwa, acha awe mdogo kama panadol.
AZIZA: Kwanza twendeni tukapate lunch, au Nyemo umeshiba?
MIMI: Nimekula home ila sijashiba wala nini. Wazo ulilolitoa liko poa. Msosi wapi?
AZIZA: Kule bondeni.
MIMI: Wanapakua kingi au nao wababaishaji.
AZIZA: Kikiwa kidogo utaongeza.
MIMI: Namna hiyo, hayo ndio maneno. Ila hapa nina 400 ya nauli tu.
AZIZA: Usijali. Nitakurudisha na gari.
MIMI: Hapo mzuka zaidi. Itakubidi uniongezee shilingi mia ninunue vocha ya 500 ili niingie facebook baadae.
AZIZA: Usijali. Nitakutumia elfu kumi kabisa.
MIMI: Duh! Sasa simu yangu si itazima
AZIZA: Kwa nini?
MIMI: Haijazoea kuingiza kiasi kikubwa cha hivyo. Sawa na mgonjwa wa Tandale ukampelekea juisi ya shilingi elfu kumi. Anaweza kufa.
AZIZA: Hahaha! Kwa nini?
MIMI: Tumbo limeingiza kitu kigeni kwa hiyo inaweza kuonekana kama asidi.
AZIZA/EDUADO: Hahaha.
MIMI: Huo ndio ukweli. Ila nina swali.
AZIZA: Swali lipi?
MIMI: Nahisi kama mnanificha. Kuna ishu inayoendelea hapa?
AZIZA: Muulize Eduado.
MIMI: Eti kaka kuna nini?
EDUADO: Aziza anakupenda. Alikuwa akikuhitaji toka zamani ila alikuwa akiogopa kukwambia, akaniambia nifanye juu chini mpaka anakupata.
MIMI: Unasemaje?
EDUADO: Ndio hivyo. Anapenda kusoma kila unachokiandika facebook, amekuwa rafiki yako mkubwa, akavutiwa na wewe ila alikuwa akikuhitaji, alichokifanya, akakuunfriend na kisha kujifanya mtu mpya kwako.
MIMI: Aiseee...duh! kwa hiyo kila kilichokuwa kikiendelea kilikuwa kikijulikana?
EDUADO: Yeah! Huo ndio ukweli.
MIMI: Sasa na wewe Aziza ulikuwa unaogopa nini kuniambia?
AZIZA: Maadili.
MIMI: Kivipi?
AZIZA: Msichana hatakiwi kumuanza mvulana.
MIMI: Hahaha! Ningekuwa na girl mwingine je?
AZIZA: Ningepigana mpaka nikupate.
MIMI: Hahaha! Aya buana. Mchezo wenu umefanikiwa na wote mmeshinda. Hebu kwanza ongezeni mwendo washikaji, unajua hapa nina ubao ile mbaya mpaka tumbo linasikia kizunguzungu.
AZIZA: Mmmh! Kwani tunatembea taratibu?
MIMI: Mnatembea kama mnamsindikiza Bibi Harusi.

Hicho ndicho kitu ambacho nilitaka kukwambia kila siku katika maisha yangu. Aziza ndiye alikuwa msichna wangu, nilimpenda na kumthamini sana. Japokuwa alikuwa msichana mwenye uwezo lakini kila alipokuwa pamoja nami alikuwa akionyesha heshima ya hali ya juu japokuwa nilikuwa nikiishi Tandale. Aziza alinipenda, nilimpenda pia, tulifanya mengi sana hasa yale ambayo wapenzi huyafanya faragha. Mpaka leo hii, bado ninampenda mtoto huyu ila cha ajabu....hahaha! hata kwao sitamani kukanyaga.

Hii ni hadithi ya kutunga, hakuna kitu chochote cha kweli. Ninapoandika facebook chatting, ni kama kuburudishana na si kufundishana kama wengine wanavyodhani. Fasihi andishi kazi yake ni kufundisha, kuonya, kuburudisha na mambo mengine. Kwa upande wa facebook Chatting, tunaburudishana tu na ndio maana hakuna hata sehemu moja kwa siku imepita bila kucheka.
Nakutakia siku njema. Kama umetokea kuipenda, unajua cha kufanya......Au hadi tukumbushane?

ASANTE KWA KAMPANI YAKO......NAMSHUKURU MUNGU KWA KUIKAMILISHA HII HADITHI JAPOKUWA TANESCO HAWAKUTAKA NIIKAMILISHE MCHANA WA LEO.

ENJOY SIKU YAKO.

MWISHO.
  •  
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger