Headlines News :

Monday, March 18, 2013

TODAY'S JOKE - DOGO


Wakati wa msosi dingi anamlazimisha dogo aombee chakula, dogo akawa hataki lakini baada ya kulazimishwa sana akaanza kuombea chakula ili wale. Akaanza: "Ee Mungu nakushukuru kwa kutubariki na kumuwezesha baba kupata hela na kutuletea chakula. Naomba umbariki na baba yake Joni mlafi ili Joni aache kuja kudowea chakula kwetu. Naomba pia umbariki Tino ambaye ni kaka yake Joni aache kuja kila siku kumvua dada nguo na
kucheza naye sarakasi kitandani wakati baba na mama wameenda kazini. Natumaini utambariki na hatacheza tena sarakasi kama kawaida yake. Naombea pia wasio na mavazi. Tafadhali wabariki na wajalie nguo wanawake wote wasio na nguo hata kidogo ambao baba amejaza picha zao katika simu yake. Hakika Baba, nao pia wanahitaji nguo kujisitiri. Mwisho kabisa naomba umpe nguo na makazi ya kudumu yule mwanaume ambaye huwa anakuja kulala na mama wakati baba akisafiri kwenda nje ya mkoa kikazi, Amen!" Hakuna mtu alikula chakula siku hiyo mwanawani. 
Patashikaaaaa la Nguvuuuuu!
  •  
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger