Headlines News :

Tuesday, April 30, 2013

UMEWAHI KUMUONA MWANAMKE MZURI KULIKO WOTE DUNIANI? KAMA BADO MCHEKI HAPA

Mwanamke Mzuri Kuliko Wote Duniani Kwa Mwaka 2013 
Huyu sio mwingine bali ni Malkia wa Saudi Arabian, aitwae Fatima Zohar-Godabari.


Fathima Kulsum Zohar Godabari ambaye awali alikuwa kwenye familia ya kifalme kwa sasa yeye ndie Malkia wa Saudi Arabia.
Hivi karibuni alipigwa picha bila kuwa amevaa niqab ikiwa imefunika uso wake, na picha hizo kuchapishwa kisha kusambazwa kwenye mitandao, zikionyesha uzuri wa sura yake duniani ikiwa ni mara ya kwanza.
Toka picha hizo zitoke, watu wengi wamekuwa wakimtaja kuwa ndiye mwanamke mzuri duniani kwa sasa.







Monday, April 29, 2013

WAJUE WANAOONGOZA KWA UTAJIRI EPL - ROONEY AONGOZA



Wayne Rooney
Mchezaji wa timu ya Manchester United na mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Uingereza Wayne Rooney, anatajwa kuwa ndiye mchezaji tajiri kuliko wote kati ya wanaocheza kwenye Ligi Kuu ya Uingereza kwa sasa.
 
Kwa mujibu wa gazeti la The Sunday Times kwenye orodha yake ya wachezaji matajiri wanaocheza kwenye Ligi hiyo kwa sasa, utajiri wa Rooney unakadiliwa kuwa ni paundi za Uingereza millioni 79.01.

Jumla ya wachezaji ishirini na nne wanaocheza kwenye ligi kuu ya Uingereza ni miongoni mwa wanamichezo 100 tajiri wa Britain na Ireland.

Utajiri wa Rooneys umepanda kwa paundi millioni sita kutoka mwaka 2012 huku akichanganya na utajiri wa mke wake Coleen ambae utajiri wake unakadiliwa kufika paundi millioni 64.

Mchezaji mwenzake wa United, Rio Ferdinand anashika nafasi ya pili, akiwa na utajiri wa paundi millioni 42 huku mshambuliaji wa klabu ta Stoke City Michael Owen akiwa ni wa tatu kwa kuwa na utajiri wa paundi millioni 38.
Utajiri huo umepimwa kwa mali zinazotambulika kama ardhi, thamani pamoja na hisa mbalimbali zilizopo kwenye makampuni.

Nahodha wa zamani wa Uingereza David Beckham, ambaye kwa sasa anaichezea Paris St Germain, anashika nafasi ya 11 ya matajiri michezo wa dunia iliyotajwa na gazeti hilo la Sunday Times, huku akikadiliwa kuwa na utajiri wa paundi millioni 165.

Mchezaji namba moja wa mchezo wa gofu Duniani Tiger Woods ndiye anayeshika nafasi ya kwanza huku utajiri wake ukikadiliwa kuwa wa paundi millioni 570.

Hii orodha ya Wachezaji 10 Matajiri wanaocheza kwenye Ligi Kuu ya Uingereza kwa sasa:

1. Wayne Rooney (Manchester United) paundi millioni 51

2. Rio Ferdinand (Manchester United) paundi millioni 42

3. Michael Owen (Stoke City) paundi millioni 38

4. Ryan Giggs (Manchester United) paundi millioni 34

4. Frank Lampard (Chelsea) paundi millioni 34

6. Steven Gerrard (Liverpool) paundi millioni 33

7. Fernando Torres (Chelsea) paundi millioni 26
8. John Terry (Chelsea) paundi millioni 24

9. Joe Cole (West Ham United) paundi millioni 21

10. Petr Cech (Chelsea) paundi millioni 20
 

(Paundi 1 =  Shilingi 2500)

PUNGUZA TUMBO NA MANYAMA UZEMBE KWA KUFANYA HAYA!!!







Its about that time of the year when you want to go for a vacation and swim in the Ocean. And you want to look mwaaaah in a swimsuit. If you are feeling a little flabby around the middle, or just want to do a little toning up, let me give you tips to get that great flat Tummy.

1. Do aerobic exercises daily. Strive for at 30 minutes a day minimum, but include one to two days of rest each week. Take up dancing, running, swimming,cycling and walking at a good pace anything that brings your heart rat

UNAYAJUA MAUMIVU YA MAPENZI? SOMA HAPA !!!

HAKUNA mwenye moyo ambaye anafurahishwa na maumivu katika mapenzi. Hapa nazungumzia usaliti, unyanyasaji, masimango na mengine mengi katika uhusiano wa kimapenzi.
Wapo watu ambao ni wa kwanza kuwaumiza wenzao lakini wao wakiumizwa ni matatizo tupu! Wanajihisi kama wao pekee ndiyo wenye moyo wa kuumia lakini wenzao hawapati maumivu. Hivi hii inaingia akilini kweli?
Marafiki zangu, lazima tufahamu kwamba mioyo yote ina nyama. Kuna mambo mengi ambayo mpenzi akifanyiwa na mwenzake lazima ataumia sana. Ingawa kuna mengine yanafichwa au kupasishwa kama sahihi, lakini ukweli unabaki pale pale kwamba yanaumiza.

Kikubwa ambacho unatakiwa kufahamu ni kwamba maumivu hayo yapo sawa kwa kila mmoja. Haijalishi jinsia, umri, kabila wala dini, maumivu ya mapenzi yote yanafanana. Kufanana huko kunasababishwa na mioyo yote kuwa na nyama!
Kwa sababu mioyo yote ina nyama basi unatakiwa kufahamu kwamba, jinsi unavyoumia wewe moyoni mwako, ndivyo mpenzi wako anavyoumia ikiwa utamfanyia makosa kama ambayo unamfanyia wewe.
 
UMEWAHI KUWAZA KUHUSU KUSALITIWA?
Unajua kabisa una mpenzi, tena inawezekana wakati mwingine mmeshawahi kuzungumza juu ya kuishi pamoja, lakini bila haya wala aibu, unamsaliti! Kwa nini unafanya hivyo? Kama umeona hana thamani tena kwako, kwa nini unazidi kumpotezea muda?
Unafikiri anafurahia sana wewe kuwa na kimada mwingine huko uchochoroni au unadhani atafurahia siku akijua kuwa una mtoto umezaa nje ya ndoa yako? Nafsi yako yenyewe inakusuta, inajua ni kiasi gani unamkosea mpenzi wako lakini unajifanya kichwa ngumu na kuendelea na uchafu wako. Kwa nini hutaki kubadilika?
Hebu jitoe katika nafasi yako, kisha mfanye mpenzi wako ndiyo wewe, halafu fikiria kama yeye ndiyo angekuwa anakusaliti, ungejikiaje? Lazima utaumia! Sasa kama utaumia kwa nini unaendelea kumfanya mwenzako akose raha?
Lazima uwe na moyo wa huruma, akili yako ifanye kazi ipasavyo na kugundua makosa unayoyafanya kisha kufanya mabadiliko ya haraka. Amini jinsi utakavyoumia kwa kufanyiwa mabaya na mwenzako ndivyo mpenzio anavyoumia kwa mabaya unayoyafanya.
Wengi wamekuwa wakiwasaliti wapenzi wao wakiwa hawafikirii siku ya wao kufanyiwa hivyo itakavyokuwa. Hebu vuta picha, unakwenda nyumbani kwa mpenzi wako, unagonga mlango haufunguliwi!

Baadaye unahisi kama ndani kuna watu, hilo linaingia akilini mwako baada ya kuona viatu vya mpenzi wako pamoja na viatu vingine vya jinsia tofauti ya mpenzi wako.
Unaamua kusukuma mlango na kuingia ndani, hamadi! Unakuta mpenzio akiwa kitandani na mtu mwingine. Utajisikiaje? Jiweke katika nafasi hiyo. Naamini kabisa ni lazima utajisikia vibaya sana, sasa kama ndivyo, kwa nini wewe unamsaliti?
Mapenzi ya kweli hayaambatani na usaliti. Penzi la kweli lina uaminifu wa dhati, kuchukuliana, kupendana, kusaidiana, ukarimu, huruma na mengine mengi ambayo huyafanya mapenzi yazidi kuwa imara kila siku.
 
USIJIFIKIRIE MWENYEWE...
Vipengele vilivyopita vinafafanua hili kwa undani, lakini kwa kuongezea ni kwamba huna sababu ya kujiwazia wewe mwenyewe! Kujiona wewe pekee ndiye mwenye haki ya kuwa salama katika penzi lako.
Chunga nafsi yako lakini wakati huo huo ukiangalia kwa jicho la tatu, nafsi ya mwenzako. Kila mmoja anaumia anapohisi kusalitiwa, hivi unafikiri ni nani anayependa kushea mapenzi? Hakuna.
Utakuta mwingine simu ya mpenzi wake ikiita anakuwa wa kwanza kuichukua na kutaka kupokea au kusoma sms, lakini subiri sasa simu yake iite; Anakuwa mkali zaidi ya mbogo! Acha kujifikiria peke yako.
 
KIPO CHA KUFANYA!
Siamini kama kuna ambacho sijaandika katika vipengele vyote vilivyopita, lakini hapa nakusisitizia kufanya mabadiliko ya haraka ili mwisho wa siku uweze kuishi maisha mapya, mazuri, yenye mapenzi ya kweli huku moyo wako ukiwa huru.
Hutakuwa na maumivu moyoni mwako, maana utakuwa unamtendea haki mpenzi wako. Lakini kama ukiendelea kumsaliti, ujue wazi kwamba utakuwa unajizidishia maumivu katika moyo wako.
Huo ndiyo ukweli!

Sunday, April 28, 2013

Subject: USED Vs. LOVED

While a man was polishing his new car, his 4 yr old son picked up stone and scratched lines on the side of the car. In anger, the man took the child's hand and hit it many times; not realizing he was using a wrench.
At the hospital, the child lost all his fingers due to multiple fractures. When the child saw his father.....with painful eyes he asked, 'Dad when will my fingers grow back?' The man was so hurt and speechless;  he went back to his car and kicked it a lot of times.  Devastated by his own actions.......sitting in front of that car he looked at the scratches; the child had written 'LOVE YOU DAD'.
The next day that man committed suicide.  Anger and Love have no limits; choose the latter to have a beautiful,  lovely life.....
Things are to be used and people are to be loved,  but the problem in today's world is that, People are used and things are loved...
During this year, let's be careful to keep this thought in mind: Things are to be used, but People are to be
loved ... Be yourself....This is the only day we HAVE.
Have a nice day and Best regards  watch your thoughts; they become words. Watch your words; they become actions. Watch your actions; they become habits. Watch your habits they become character; Watch your character; it becomes your destiny.

I hope you are having a wonderful day!

KWA MASHABIKI WA MAN UTD, HII NI YENU TENA

Wachezaji wote wa Man United kupata medali za EPL.

image
Wachezaji wote wa mabingwa  wapya wa ligi kuu ya England watapata medali za ubingwa wa ligi kuu ya England baada ya chama cha soka che England na ligi kuu kulegeza masharti yaliyokuwa yanabana idadi ya wachezaji wanaoweza kupewa medali pale timu inapotwaa ubingwa .

Katika misimu ya miaka ya nyuma wachezaji waliokuwa wanaweza kupewa medali baada ya timu kuwa bingwa ni wale waliocheza idadi ya mechi 10 na zaidi huku magolikipa pekee wakiwa na nafasi ya upendeleo , zaidi ya hapo kama idadi ya medali ni ndogo timu ilikuwa inatakiwa kutuma maombi maalum abayo yalihitaji kuridhiwa na FA ya medali za ziada .

Hata hivyo kwa sheria mpya ya ligi kuu ya England wachezaji wanaoweza kuvaa medali ni wale waliocheza mechi tano ha zaidi huku timu inayotwaa ubingwa ikipewa medali 40 na kutakiwa kutuma maombi kwa wale wanaoweza kuwa wamekosa medali hizo.

Kwa sheria za zamani wacheza Darren Fletcher , Alexander Buttner  na Nick Powell wasingeweza kupewa medali huku kipa Anders Lindergaard akipata kwa sababu sheria hiyo ilikuwa haiwahusu makipa , hata hivyo kwa sasa wachezaji hawa watapata medali kama kawaida huku kukiwa na nyomgeza ya kutosha kuwapa wachezaji wengine wa kikosi cha kwanza ambao hawapati nafasi za kucheza kama Ben Amos,Jesse Lingard , na Marnick Vermijl na mchezaji Adnani Januzaj ambaye anacheza kwenye kikosi cha U-18 ambaye amepewa jezi namba 44 huku kocha Sir Alex Fergusson akiahidi kumpa nafasi kwenye mechi zilizobaki.

Fergie ameipa dole sheria hiyo akisema kuwa iko ‘fair’ kwa kuwa kila mchezaji hata kama amecheza mechi tatu kama kina Powell,Fletcher na Buttner anahesabika kuwa ametoa mchango unaostahili medali.

JINSI YA KUMKABILI MWANAUME ASIYE CHAGUO LAKO!

Ni kweli kwamba, kila binadamu ana haki ya kupenda, hili halipingiki hata kidogo, lakini kulingana na mila na desturi zetu za Kiafrika wanaume ndio huwa waanzilishi wa uhusiano.
Kwa utamaduni huo basi, mwanamke hukosa uhuru wa kufikisha hisia zake kwa yule aliye chaguo lake huku mwanaume akiwa huru kutoa dukuduku lake pale anapohisi kupenda.
Pamoja na kwamba maendeleo ya sayansi na teknolojia yanamfanya mwanamke wa sasa awe na haki sawa na mwanaume, bado kumekuwa na ugumu kwa mwanamke kumwambia mwanaume kuwa anampenda na angependa kuwa mpenzi wake.
Mwanamke wa aina hiyo, huonekana mhuni, asiyejiheshimu. Lakini kuna jambo moja la msingi hapa kulijadili; ni pale mwanamke anapotongozwa na mwanaume asiye chaguo lake. Wakati mwingine inawezekana hata hajatongozwa, lakini dalili za mwanaume huyo zikamfanya aone wazi kwamba anamtaka ila yeye moyoni mwake akawa hana nafasi kabisa.
Hapa ndipo wanawake wengi wanapobaki njia panda. Kwa bahati mbaya sana, wapo ambao huamua kuingia kwenye uhusiano kwa majaribio, jambo ambalo ni hatari kwenye uhusiano.
Inapotokea hali hiyo baadhi ya wanawake wanashidwa kujua la kufanya na kufikiri labda kuwajibu majibu ya hovyo huweza kufikisha hisia zao na kuachwa kusumbuliwa.
Kama yupo mwanaume anayekusumbua mara kadhaa na wakati mwingine kuona kuwa ni kero kwako na hujui cha kufanya, usijali fungua ubongo ili uweze kuongeza kitu kipya. Kuna baadhi ya wanawake wanafikia hatua ya kuwatukana au kuwakejeli wanaume ambao wamekuwa wakiwasumbua kila wakati.
Usijali, kipo kitu cha kufanya. Zipo njia za kumweleza mwanaume husika humhitaji kistaarabu na yeye asijisikie vibaya na ukamuacha akiwa mwenye kukuheshimu siku zote za maisha yake.

NI MWANAMKE YUPI?

Thursday, April 25, 2013

VIGEZO 10 VYA KUMPATA MUME/MKE /MCHUMBA MWENYE MAPENZI YA KWELI

Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Ramla aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Na leo my best friend na mdau wangu mkubwa wa Blog hii  Rayha ametaka kujua vigezo gani vya kuzingatia ili kumpata mume/mpenzi borana mwenye mapenzi ya kweli na ya dhati , hii ameiandika kwenye ukurasa wake wa facebook.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.

Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

KAMA NI MWANAO ANAKUAMBIA HIVI , JEE UTAMJIBU NINI?

Mom, I've got a secret
But I'm not sure if I'm ready to tell
When I whisper it in your ear
Please don't say I'm going to hell

Please treat me like your daughter
I need to know that you accept
Don't make me think that the truth
Is a secret I should've kept
Maybe you'll still love me...

I'm just letting my hopes get too high
But I'm not sure how long I can keep this up
There is hurt with every lie
Maybe if I tell you
You'll join me in silence this year

This secret is so hard to let out
It's your hate that I fear
Will you still love me?
Or will things between us change?
I know that once I tell you

Your views about me will be rearranged
Before I share my secret
I wanna know what you'll do or say
So let me ask you this question;

Mom, will you still love me if I'm gay?

COMMENT HAPO CHINI BILA KUHARIBU HALI YA HEWA





Sunday, April 21, 2013

PUNGUZA CHUNUSI


Chunusi husababishwa na kuongezeka kwa uzalishaji wa Testosterone hormone na mafuta yamwili wakati wa mabadiliko ya kimwili pia husababishwa na msongo wa mawazo, matatizo ya kisaikolojia.
Ili kuepuka chunusi hizo fanya mambo yafuatayo.
  •  Product kama Tea Tree Oil, Aloe Vera, Zinc, and Vitamin A ni vitu vya kihalisi vinavyo weza kutibu chunusi na kuna baadhi ya product hazishauriwi kutumiwa na mtu kama unaujauzito au unatatizo la kiafya hivyo unatakiwa kuwasiliana na dactari kabla ya kutumia kwa ushauri.

UREMBO - JINSI YA KUTUNZA NYWELE KWA VITU ASILI

Leo katika somo letu la urembo ningependa kuangalia katika utunzaji wa nywele bila ya kujihusisha na matumizi ya madawa ya kemikali ambayo yamesababisha kwa kiwango kikubwa matatizo katika ukuaji wa nywele kama nywele kukatika,kunyonyoka,kupooza katika ukuaji n.k
Hina ni moja kati ya mimea ambayo watu wengi hasa wanawake huitumia katika kujiremba hasa kujichora maungoni bila kutambua kuwa mmea huo huweza kusaidia katika utunzaji wa nywele zao pia kwa kiasi kikubwa.

Hebu tuanze maandalizi ya Hina.

 MAHITAJI:-

Wednesday, April 17, 2013

BREAKING NEWS!!!!!!

 

BI KIDUDE AFARIKI DUNIA.


Bi Kidude 7a829
Mwanamuziki gwiji nchini Fatuma Binti Baraka "Bi Kidude" hatunaye tena. Taarifa toka kwa familia yake zinasema Bi Kidude aliekuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Hindu Mandal amefariki leo. Bi Kidude atakumbukwa kama mwanamuziki mkongwe zaidi nchini ambaye alianza muziki akiwa na umri wa miaka 10 tu na aliwahi kupokea tuzo mbalimbali kutokana na mchango wake katika muziki wa mahadhi ya mwambao. Hakika sanaa nchini imepoteza moja ya nguzo kubwa.
Pumzika kwa amani Fatuma Binti Baraka.
  • World News

     
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger