Headlines News :

Monday, June 16, 2014

UNAAMBIWA HUYU NDIO NGAMIA ANAYETABIRI MECHI ZA KOMBE LA DUNIA - BRAZIL 2014

20140616-102950-37790371.jpg
Kwenye miaka ya hivi karibuni kumekuwepo na matumizi ya wanyama na viumbe wengine kwenye kutabiri matokeo ya mechi za soka hasa kwenye michuano mikubwa kama kombe la dunia.
Mwaka 2010 wakati wa WOZA, nchini Ujerumani kulikuwa na Pweza ‘Octopus Paul’ ambaye alitabiri mechi zote na akapatia kila utabiri, mwaka huu amekuja Ngamia aitwaye Shakeeen kutoka Dubai ambaye nae alianza kutabiri tangu siku ya kwanza.
Shakeen ambaye anamilikiwa na shabiki mmoja wa timu ya soka ya Al Wasry ya Dubai, alitabiri mechi zote za ufunguzi na akapatia, akatabiri ushindi wa Italy dhidi ya England akapatia, jana akaitabidi ushindi Ufaransa na Argentina akapatia tena.
Pia ameitabiria Ureno kushinda mechi ya leo dhidi ya Ujerumani.
20140616-103044-37844157.jpg
  • World News

     
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger