Headlines News :

Monday, September 30, 2013

CHOMBEZO : FACEBOOK CHATTIN' - 8



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
SIMU: 0718 069 269.
FACEBOOK CHATTING 8



Aziza alionekana kama kupigwa ganzi, hakujua ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati huo, nilimuona akianza kutetemeka huku kwa mbali kijasho chembamba kikianza kumtoka. Hakuonekana kuamini kile ambacho alikuwa akikiona mahali pale.

MIMI: kwa hiyo?
AZIZA: Sijui nifanye nini.
MIMI: Chumba chako kipo wapi?
AZIZA: Njoo.

Nikaanza kumfuata kule aliponiambia nimfuate, chumbani. Nilijua fika kwamba katika kipindi hicho akili yake haikuwa sawa, mimi kama ninja nikatakiwa kufanya manuva. Tukaenda mpaka chumbani kwake, alikuwa akiendelea kutetemeka tu. Baada ya kufika chumbani, mtu mzima nikabaki nikikiangalia chumba kile, kilionekana kuwa na mvuto sana.

AZIZA: Kwa hiyo.
MIMI: Daah! Ngoja nizame chini ya kitanda (Mtu mzima nikazama chini ya kitanda)

Huko chini kulionekana kusafi ajabu, kitanda kile kikubwa cha chuma kilikuwa na nafasi ya kutosha kabisa. Kitu cha kwanza nilichokifanya ni kuichukua simu yangu na kisha kuiweka katika Silent. Nilibaki nikijiuliza sana kwamba kwa nini jambo kama lile lilikuwa likinitokea? Kwa nini Aziza alikuwa ameniaminisha sana mimi kwenda kwao mpaka kutaka kuniletea msala? Kila nilichojiuliza nikakosa jibu. Kule chini ya kitanda nikaanza kuchati na Eduado kupitia sms za kawaida.

EDUADO: Nyemo umefikia wapi?
MIMI: Kaka acha. Nipo kwao.
EDUADO: Du! Upo kwao? Wewe noma. Ilikuwaje kuwaje hadi umefika kwao?
MIMI: Alikuja kunichukua home.
EDUADO: Sikupatii picha mtu mzima. Leo malovee hapo hapo chumbani kwake.
MIMI: Haha! Kaka acha. Nipo uvunguni.
EDUADO: Uvunguni! Kivipi tena?
MIMI: Baba yake amefika na wakati dogo alisema kwamba anarudi saa mbili usiku. Karudi kwa kushtukiza, yaani hapa nimeingia chumbani kwake na kujificha uvunguni.
EDUADO: Hahaha! Kaka hiyo kweli noma, sikupatii picha aisee ulivyojipinda huko mtu mzima.
MIMI: Kaka wewe acha tu, huku ni noma. Ukisikia nimepigwa risasi, usishangae.
EDUADO: Dah! Ngoja nikuombee Mungu akuokoe.
MIMI: Wewe unafikiri Mungu atanisaidia hapa?
EDUADO: Atakusaidia tu.
MIMI: Kunisaidia anaweza ila dah! Kaka mimi ni mwenye dhambi. Nafikiri atataka nikamatwe ili nisirudie mchezo wangu.
EDUADO: Kaka pole sana. Sasa mtoto anasemaje?
MIMI: Yaani hapa ni kujiokoa mwenyewe. Aziza anazingua, anaonekana kuogopa sana.
EDUADO: Kwa hiyo utatokaje humo uvunguni?
MIMI: Ngoja kwanza giza liingie manake huku mtu unaweza kufa.

Mtu mzima nilikuwa nazidi kutetemeka chini ya uvungu wa kitanda, Aziza hakuwa akitulia, mara aingie, mara atokea hali ambayo ikanionyeshea angetoa boko muda wowote ule. Nilichokifanya nikachukua simu yangu na kisha kuanza kumtumia meseji.

MIMI: Nini kinaendelea hapo?
AZIZA: Baba amekaa sebuleni, amekuja na wageni. Tena wageni ambao watalala hapa hapa nyumbani.
MIMI: Hilo sio tatizo sana. Wa kike au wa kiume?
AZIZA: Wa kike.
MIMI: Duuh! Ila si watalala chumba cha wageni?
AZIZA: Yeah! Ila wengine watalala katika chumba changu. Mbaya zaidi baba ameniambia nije kusogeza kitanda ili kiingizwe kitanda cha pili.
MIMI: Duuuh! Leo kazi ipo.
AZIZA: Mbaya zaidi amemwambia mdogo wangu aje kufagia chumbani.
MIMI: Mungu wangu! Nimekwisha.
AZIZA: Naomba uniambie nifanye nini Nyemo.
MIMI: Kwanza kabla ya yote punguza presha.
AZIZA: Sawa.
MIMI: Najua kwamba leo nakwenda kukamatwa, kabla sijakamatwa naomba uniambie kitu kimoja.
AZIZA: Kitu gani?
MIMI: Unanipenda?
AZIZA: Nakupenda Nyemo.
MIMI: Upo tayari tuingie katika mahusiano kwa muda mchache uliobakia kabla sijauawa na baba yako?
AZIZA: Nyemo usiseme hivyo.
MIMI: Wewe unafikiri nitasemaje? Naomba unijibu. Upo tayari?
AZIZA: Nipo tayari lakini jua hautokwenda kuuawa.
MIMI: Nimefanya kila kitu kwa ajili yako, nilihisi mambo haya yatatokea tu toka tulipokuwa tukija. Ila usijali. Ngoja nikuonyeshe jinsi mchezo unavyofanyika Aziza. Nataka nikuonyeshe kwamba huwa sikamatwi kijinga jinga.
AZIZA: Utafanya nini sasa?
MIMI: Cha kwanza hakikisha mdogo wako haji kusafisha chumba, akifika chumbani mpokonye fagio, ng’ang’ania kusafisha chumba chako.
AZIZA: Sawa. Cha pili?
MIMI: Hakikisha kila unapotoka chumbani, unafunga mlango kwa ufunguo, cha tatu, uache mlango wa jikoni wazi, cha nne mpe taarifa baba yako kwamba kuna mtu alikuja kumuulizia.
AZIZA: Mmmh! Huyo mtu nani?
MIMI: Nyemo...ila leo niite jina la Ahmed.
AZIZA: Akisema yupo vipi?
MIMI: Mwambie kama jinsi nilivyo. Usitie shaka.
AZIZA: Kingine nisemeje?
MIMI: Mwambie kwamba ningekuja baadae kumuulizia tena.
AZIZA: Mhh!
MIMI: Usijali. Kila kitu kipo under control.
AZIZA: Sawa.

Baada ya dakika kadhaa, nikasikia mlango ukifunguliwa, nikasikia vishindo vikija kwa kasi, alikuwa mdogo wake ambaye alitaka kusafisha chumba kwa kukifagia, Aziza akafika na kisha kumpokonya ufagio kwa kutaka kufagia yeye mwenyewe. Mdogo wake alipoondoka, akakiinamisha kichwa na kisha kukutana nami.

MIMI: Vipi huko?
AZIZA: Bado hali ni ngumu.
MIMI: Daah! Sikamatwi kijinga hapa. Fanya kama nilivyokwambia, umesikia?
AZIZA: Sawa.
MIMI: Nakupenda mpenzi.
AZIZA: Nakupenda pia (Tukafanya kile tulichotaka kukifanya pale sebuleni....lol)

Aziza akaondoka, nikaona sio ishu, niliendelea kukaa uvunguni mule. Nazo dakika zilikuwa zikisogea tu, zilisogea zaidi na zaidi, mpaka saa moja usiku inaingia, mtu mzima nilikuwa mule mule ndani chini ya uvungu. Saa mbili kasoro nikaona ungekuwa ujinga, nikamtumia Aziza meseji.

MIMI: Njoo uvunguni kwanza.
AZIZA: Sawa.
MIMI: Ila kabla ya kuja, cheki kuna nani jikoni.
AZIZA: Yupo mama.
MIMI: Vizuri sana
AZIZA: Vizuri?
MIMI: Yeah! Njoo kwanza huku uvunguni.

Baada ya muda, Aziza akafika, hakuonekana kuwa na amani.

AZIZA: Unasemaje baby?
MIMI: Hapa naondoka na kuelekea jikoni, cha msingi kamtoe mama yako jikoni.
AZIZA: Mmmh! Nitamtoa vipi?
MIMI: Kamwambie kwamba baba yako anamuita.
AZIZA: Eeeh!
MIMI: Fanya hivyo. Una dakika moja ya kufanya hivyo. Nakwenda kwa muda.
AZIZA: Hlafu?
MIMI: Wewe kamwambie hivyo. Akija sebuleni mimi utanikuta nje ambapo huko sebuleni utamwambia baba yako kwamba kulikuwa na mtu alikuja kumuulizia. Umesikia
AZIZA: Na mama akifika sebuleni na kusema kwamba kaitwa kumbe hajaitwa?
MIMI: Mwambie uliskia vibaya.
AZIZA: Sawa.
MIMI: Kenye ile dakika moja, umebakisha sekunde arobaini. Nenda, ukitoka zima taa ya humu chumbani na uuache mlango wazi kidogo
AZIZA: Sawa.

Aziza akaondoka mahali hapo, na kweli akaelekea jikoni na kumwambia mama yake kwamba alikuwa akiitwa na baba yake, nilipomuona mama yake akipita ukumbini kueleka sebuleni, alipopita, nikaufungua mlango na kupita kuelekea jikoni, nikaufungua mlango na kutoka nje kwa nyuma, nikaanza kuambaa ambaa mpaka pembeni ya gari lao.

MAMA AZIZA: Nimekuja mume wangu.
BABA AZIZA: Kuna nini?
MAMA AZIZA: Aziza amekuja na kuniambia unaniita.
BABA AZIZA: Mimi! Hapana, labda kasikia vibaya.
AZIZA: Si nimesikia unamuita mama.
BABA AZIZA: Hapana.
AZIZA: Basi samahani nilisikia vibaya
MAMA AZIZA: Usijali. Nipo jikoni naandaa chakula kwa sababu dada wa kazi anaumwa, amelala na huyu Aziza asije akatoa chakula kibichi
BABA AZIZA: Sawa. Aziza, wapeleke chumbani wageni hawa.
AZIZA: Sawa. Ila leo kuna mtu alikuja kukuulizia.
BABA AZIZA: Nani?
AZIZA: Sijui, ila alisema atarudi usiku.
BABA AZIZA: Yupo vipi?
AZIZA: Mrefu kidogo, maji ya kunde halafu ana.........!

MLANGO: Ngo ngo ngo ngo (Nilikuwa nikipiga hodi huku mlinzi akionekana kunishangaa kwani aliniona ninavyoingia na Aziza, alikuwa hajui sababu kwa nini nilikuwa nimetokea nyuma ya nyumba na kuanza kugonga mlango. Mlango ukafunguliwa, alikuwa Aziza, kama vile sterring, nikaingia ndani, Baba yake Aziza akabaki akiniangalia, sikufichi, nilijiamini kama Van Damme)

Itaendelea kesho.
  •  
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger