Headlines News :

Friday, September 27, 2013

CHOMBEZO : FACEBOOK CHATTIN' - 5



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
FACEBOOK CHATTING 5
0718 069 269


Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa upande wake, nikaona ukimya ukiwa umetawala mahali hapo, nikawa naisubiria meseji yake huku nikionekana kuwa na kiu kubwa ya kutaka kusikia kitu chochote kutoka kwake, hasa jibu la swali ambalo nilikuwa nimemuuliza.

AZIZA: Mhh!
MIMI: Nini tena?
AZIZA: Una haraka sana Nyemo. Maswali yako mengine yanakufanya nikuone mtu wa haraka mno.
MIMI: Tatizo muda Aziza. Nahofia kwamba nikichelewa, nitakuta ushachukuliwa kitu ambacho sitaki kitokee.
AZIZA: Hahaha! What if nikisema sikupendi?
MIMI: Nafikiria litakuwa neno baya ambalo sijawahi kulisikia katika maisha yangu.
AZIZA: Hahaha! Nyemo una maneno sana. Hivi unayatoa wapi hayo yote?
MIMI: Kutoka moyoni mwangu Aziza. Nimetokea kukupenda sana.
AZIZA: Lakini bado mapema sana.
MIMI: Najua. Najua kwamba mapema ila kumbuka kwamba vitu vingine ni lazima vifanyike mapema. Nadhani sina makosa juu ya hilo.
AZIZA: Nikuulize swali?
MIMI: Niulize.
AZIZA: Una mpenzi?
MIMI: Nadhani ningekuwa na mpenzi nisingeweza kukwambia kwamba nakupenda na kukuhitaji.
AZIZA: Kwa nini usiweze?
MIMI: Uaminifu. Napenda sana kuwa mwaminifu hasa kwa mtu nimpendae.....thats all.
AZIZA: Sawa. Ila mbona haujaniuliza kama nina mpenzi au la?
MIMI: Nadhani sitakiwi kujua kwani kwa upande mwingine nikitokea kujua, nitaumia kitu ambacho sitaki kitokee moyoni mwangu.
AZIZA: Nakuonea huruma Nyemo.
MIMI: Kwa nini?
AZIZA: Unampenda mtu usiyewahi kumuona.
MIMI: Hahaha! Hilo si tatizo Aziza. Kukuona haijalishi,. Kitu kinachojalisha ni wewe na mimi kuwa pamoja tu.
AZIZA: Sasa kama nina mpenzi itakuwaje?
MIMI: Sijajua itakuwaje lakini kitu ninachokihitaji ni kimoja tu, kupata nafasi moyoni mwako, kuthaminiwa na kupewa kipaumbele.
AZIZA: Kwa hiyo mpenzi wangu nimuache kwa sababu yako?
MIMI: Simaanishi hivyo Aziza.
AZIZA: Hiyo ndio maana yake. Yaani nimuache mpenzi wangu.
MIMI: Wakati mwingine inawezekana. Ngoja nikupe kijistori cha kizushi.
AZIZA: Aya nipe.
MIMI: Kuna mwanamke mmoja alikwenda kuchota maji siku moja, alikuwa amechoka na kuchafuka sana. Sehemu alipokuwa amechota maji kulikuwa mbali sana, kichwani alikuwa na ndoo na mkononi alikuwa na kidumu. Bahati mbaya, akajikwaa, ndoo ikadondoka na kupasuka, maji yakamwagika na kushindwa kuzoleka.
AZIZA: Dah! Alifanya nini sasa?
MIMI: Kurudi bombani kulikuwa mbali sana na alikuwa amechoka kupita kawaida. Kile kidumu ambacho alikuwa nacho mkononi ndicho kilichomsaidia kuoga.
AZIZA: Stori nzuri.
MIMI: Yeah! Ni nzuri na iliyojaa mafunzo. Umejifunza nini?
AZIZA: Nimejifunza kwamba yatupasa kuwa na kidumu pia katika kipindi tunachokwenda kuchota maji.
MIMI: Umekuwa mwerevu sana. Nadhani ushajua nimemaanisha nini.
AZIZA: Hahaha! Kumbe ndio umemaanisha hivyo? Yaani nina ndoo na unataka niwe na kidumu?
MIMI: Yeah! Ila naomba ufahamu kitu kimoja. Wakati ndoo inapovunjika, kidumu kitaweza kufanya kazi kama ndoo. Kwa hiyo ni muhimu kuwa na kidumu pia japokuwa haulazimishwa kufanya hivyo.
AZIZA: Nyemo unanifundisha tabia mbaya.
MIMI: Hapana. Sikufundishi tabia mbaya ila nakupa tekniki nyingine ya maisha. Njia ambazo unaweza kufanya plan B mara plan A inapoonekana kuharibika.
AZIZA: Ok! Nimekuelewa.
MIMI: Sasa umechukua hatua gani baada ya kunielewa?
AZIZA: Inabidi unipe muda wa kufikiria kwanza manake duh! Kuwa na kidumu inahitaji moyo.
MIMI: Nisikilize Aziza. Unataka kwenda kuomba ushauri wapi? Kwa mama?
AZIZA: Hapana Nyemo, ila nahitaji kujifikiria juu ya hilo.
MIMI: Kwani moyo wako unakwambia nini sasa hivi juu yangu?
AZIZA: Hauniambii kitu chochote.
MIMI: Unanidanganya Aziza. Hautakiwi kulifikiria jambo hili, unapoamua kufanya maamuzi ya maisha yako yakutakiwa kuwa peke yako Aziza.
AZIZA: Najua. Sasa wewe unafikiri natakiwa kumuomba ushauri nani zaidi ya mama?
MIMI: Niombe ushauri mimi.
AZIZA: Hahaha! Aya basi nishauri juu ya hili. Unaonaje, niwe na Nyemo au?
MIMI: Hahah! Ninachokushauri ni kwamba inakupasa kuwa nae kwani kwa muonekano wake tu anaonekana kukupenda na kukuhitaji sana tofauti ya unavyofikiria Aziza. Usimuumize, mpende, kama ameamua kukupenda, kuutoa moyo wake kwa ajili yako, mfanyie the same.
AZIZA: Hahaha! U mshauri mbaya sana.
MIMI: Kwa nini?
AZIZA: Unanishauri vitu vibaya. Ila ok! Naomba nikufikirie kwani sitaki kukuumiza. Nikisema nitoe jibu langu sasa hivi, utaumia na mimi sitaki uumie.
MIMI: Sawa. Kama unaona ukitoa jibu la papo kwa papo utaniumiza, basi usifanye hivyo. Kwa hiyo lini utanijibu.
AZIZA: Wewe unataka lini?
MIMI: Sasa hivi....lol!!
AZIZA: Utaumia. Naomba unipe muda. Bado tuna nafasi kubwa ya kuzidi kuwasiliana Nyemo.
MIMI: Poa. Kama ndio hivyo hakuna noma, acha tuzidi kuwa na nafasi zaidi.
AZIZA: Umekasirika?
MIMI: Hapana. Sijakasirika. Kwani umeongea neno lolote la kunikasirisha?
AZIZA: Hapana ila wanaume wengine huwa ukiwakataa wanakasirika sana na kesho wanakuwekea post.
MIMI: Acha nao. Hawajui mapenzi, mapenzi yanahitaji subira, mapenzi yanahitaji kujitoa kwa kila kitu, hautakiwi kukata tamaa ila mapenzi pia yanahitajiiiii........
AZIZA: Yanahitaji nini?
MIMI: Kuyafuatilia sana kama unafuatilia kazi.
AZIZA: Hahaha! Una maneno wewe mtoto.
MIMI: Kawaida tu. Ila kiukweli...dah! hongera.
AZIZA: Hongera ya nini?
MIMI: U mzuri sana. Yaani dah! Sijui niseme nini. Kuna mengine nikisema naona kama nitaonekana muongo.
AZIZA: Hahaha! Kivipi? Niambie tu.
MIMI: Jana nilipokuwa nikinywa maji, nilikuona kwenye glasi, nilipokuwa najitazama kwenye kioo, nilikuona wewe. Usiku silali, nakuota wewe tu.
AZIZA: Hahaha!
MIMI: Maneno ya zamani hayo. Wanawake wa zamani ulikuwa ukiwaambia hivyo....fasta unamchukua. Ila nyie wa siku hizi mmejanjaruka sana.
AZIZA: Hahaha! Kwa sasa hivi tunajua ukweli kwamba huwezi kuniona kwenye maji.
MIMI: Ok! Tuachane na hayo. Hivi tunaweza kuonana?
AZIZA: Kuonana. Mbona mapema sana!
MIMI: Poa, usijali. Tutaonana tukizeeka kwa sababu ndio utakuwa muda muafaka.
AZIZA: Hahaha!
MIMI: Hiyo ndio maana yake. Yaani kuonana tu unataka tupeane kalenda. Kweli makubwa.
AZIZA: Usijali. Tutaonana soon. Ngoja nikamilishe vitu fulani hivi vya kifamilia.
MIMI: Ok! Hakuna tatizo. Unaweza kuchukua muda gani?
AZIZA: Si muda mrefu, kama siku mbili tatu hivi. Unatamani kuonana na mimi?
MIMI: Yeah! Ninatamani sana Aziza.
AZIZA: Ok! Hakuna tatizo. Utaonana na mimi kwa masharti.
MIMI: Masharti gani?
AZIZA: Uje nyumbani.
MIMI: Mh!
AZIZA: Nini tena?
MIMI: Kwa nini usije nyumbani. Au unaogopa matope, unaogopa kuchafuka kutokana na matope ya uswahilini?
AZIZA: Hapana. Nitakuhitaji uje nyumbani.
MIMI: Unataka nife nini?
AZIZA: Kwa nini?
MIMI: Baba yako. Nadhani ataniua.
AZIZA: Usijali. Ninapokwambia uje nyumbani, namaanisha kwamba siku hiyo itakuwa poa na hakutokuwa na tatizo.
MIMI: Sawa. Ukiwa na nafasi naomba uniambie. Shida yangu nikuone tu.
AZIZA: Sawa. Usijali. Tutaonana tu.

Siku hiyo tulichati sana mpaka saa saba usiku muda ambao alitaka kulala, niliridhika na hivyo kumruhusu kwa moyo mmoja kulala. Siku zikakatika mpaka kufikia siku ambayo Aziza akataka kuonana na mimi. Nakumbuka siku hiyo ilikuwa kama ndoto kwangu, baada ya miezi miwili ya mawasiliano bila kuonana leo hii Aziza akaniambia kwamba alikuwa akitaka kuniona, nilitamani kuruka ruka kwa furaha.
Siku ya tukio ilipofika, nikaoga na kujiweka makini, nikachukua jinzi yangu na kuivaa, nikachukua raba zangu za kawaida na kuzivaa huku kofia yangu ikiwa kichwani mwangu. Kutoka nyumbani mpaka kwao Masaki wala hakukuwa mbali, nilitegemea kuchukua daladala na hatimae kwenda nyumbani kwao. Mara baada ya kumaliza kujiandaa, nikaingia facebook na kisha kuanza kuwasiliana nae.

MIMI: Nipo tayari.
AZIZA: Ok! Chukua namba yangu. Hii hapa. 0718 069 269.
MIMI: Ok! Ndio najiandaa kwenda kituoni sasa hivi.
AZIZA: Kwani umeshatoka nyumbani?
MIMI: Bado.
AZIZA: Basi usijali. Nielekeze nije kukuchukua.
MIMI: Uje kunichukua?
AZIZA: Yeah! Kuna ubaya?
MIMI: Yeah! Sijawahi kufuatwa na gari toka nizaliwe.
AZIZA: Usijali. Leo nitakuwa wa kwanza kukufuata. Umesema Tandale, napafahamu kidogo, nitakuja mpaka kwa Mtogole then unielekeze.
MIMI: Hakuna tatizo. Nakusubiria.

Sijui niseme nini aisee, huyu mtoto alikuwa akijiandaa kuja kunichukua nyumbani kwa ajili ya kuelekea nyumbani kwao, nilikuwa na presha sana, sikuwa nikijiamini kwamba nilikuwa mimi Nyemo. Moyo wangu ukawa na dukuduku kupita kawaida, mavazi niliyoyavaa niliyaona kutokuwa fresh hali iliyonifanya kubadilisha mara kwa mara. Sikujua Aziza alikuwa akifanana vipi, uzuri ambao aliusema Eduado, leo nilikuwa nakwenda kuuona kwa macho yangu.

Je nini kitaendelea?
Je huyu Aziza ni mzuri kweli au napo nimeuziwa mbuzi kwenye kiroba kama kwa Sikitu?
Itaendelea  . . .
  •  
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger