Headlines News :

Wednesday, September 25, 2013

CHOMBEZO : FACEBOOK CHATTIN' - 3



Sikutaka kuleta shobo tena kwani tayari nilimuona kuku kuwa wangu kwa hiyo sikutakiwa kumshikia manati kwa kuamini kwamba jioni ikifika mwenyewe atarudi bandani. Nilipoingia online siku iliyofuatia, msichana Aziza alikuwepo, kajaa tele ila mtu mzima nikaamua kuchuna. Katika hili ngoja nikwambie kitu kimoja rafiki yangu hasa mwanaume kama mimi. Unapoona kwamba kuna msichana fulani unampigia sana misele facebook, hautakiwi kila wakati umuanze wewe tu, sometimes unamchunia uone je ataweza kukutumia meseji au la. Ukiona kwamba kakutumia, basi jua kwamba anautambua mchango wako na hata kwenye ile mishemishe yako anaonekana kuifurahia. Ila ukiona nae anakaa kimya, mtu mzima poteza kwani si unajua warembo wapo wengi! Inawezekana haujapangiwa kuwa na huyo.
Nilipomuona Aziza online, nikamchunia kana kwamba sijamuona huku nikiamini kwamba yeye ndiye alipaswa kunitumia meseji. Ila katika kipindi hiki hasa siku ya leo, meseji zilikuwa zikiingia nyingi nyingi hasa kutoka kwa marafiki zangu wengine, bahati nzuri nilikuwa natumia kompyuta hivyo ilikuwa rahisi kuwajibu.

IBRA: Mambo vipi kaka!
MIMI: Poa. Ni aje mkuu?
IBRA: Kama kawa. Upo wapi?
MIMI: Nipo gheto aiseee nimesizi tu si unajua kijimvua nje kinazingua.
IBRA: Yeah! Hilo kweli kaka. Hivi unamuona mtu wangu hapo online?
MIMI: Nani?
IBRA: Tina.
MIMI: Dah! Hapa namuona kwa kuotea, mara anakuja mara anatoka. Kama vipi mcheki kwa whatsapp.
IBRA: Kwani yupo huko?
MIMI: Yeah!
IBRA: Dah! Basi nafikiri kule atakuwa kaniblock mtu mzima. Simuoni kabisa.
MIMI: Hahahah! Kaka pole sana. Umeblockiwa...hahaha! Tatizo lako uliremba sana kwa kujifanya umeoa, full mauhakika.
IBRA: Unajua nini kaka, kila siku naamini kwamba mwenda pole ndiye mla nyama.
MIMI: Usitake kuniambia hivyo. Wahenga wengine walikuwa wakizingua tu, kidogo naweza kumuamini yule aliyesema chelewa chelewa utakuta mwana si wako. Si kwamba unamuona kinyonga anatembea taratibu ukajua hata yeye anajua kwamba anatembea taratibu, mwenzako pale anajiona anakimbia kwa kasi sana. Hahahaha! Na bado...atakublock mpaka facebook.
IBRA: Akiniblock na hapa tena, nitamuona katili sana kaka.

Huku nikiendelea kupiga stori na Ibra, mara Emmanuel Solo nae akaingia kwa inbox yangu. Sikuwa na jinsi, nilikuwa nachati nao huku nikimuona Aziza online ila nami nilikuwa nimemlia pini tu.

SOLO: Kaka.
MIMI: Niambie.
SOLO Upo wapi?
MIMI: Nipo gheto. Wewe upo wapi?
SOLO: Nipo Morogoro kama kawaida yangu.
MIMI: Duh! Wewe noma. Ndani ya wiki moja umetembea mikoa mitatu. Big Up mkuu.
SOLO: Kutafuta kaka. Maisha kutafuta. Si unamuona hata Ndimanga Hassan, anatembea zaidi ya mikoa kumi kwa mwezi, hatutakiwi kukaa sehemu moja. Hadithi imeishia wapi?
MIMI: Ipi? Zipo nyingi tu.
SOLO: Ile ya yule msichana mwimbaji wa kwaya aliyekuwa amepanga mauaji kwa mvulana ambaye alikuwa amemkataa kanisani na kuamua kutaka kumuua nchini Zambia.
MIMI: Bila shaka unaizungumzia HER HIDDEN FACE, si ndio?
SOLO: Yeah!
MIMI: Ile ipo sehemu ya tano. Inaendelea kama kawa.
SOLO: Basi poa. Ngoja niitafute niendelee kuisoma.

EDUADO: Kaka
MIMI: Niambie kijana.
EDUADO: Mtoto leo kaja chuo aisee kapendezaje!
MIMI: Acha utani.
EDUADO: Sure. Mtoto ni noma kaka. Mtoto mrembo mpaka anajishangaa. Namuona online, ushatupia mambo?
MIMI: Hapana. Nangoja anianze, asiponianza nampotezea tu kwani si lazima kivile kuchati nae na kumshobokea.
EDUADO: Ila kaka fanya mambo bhana. Huyu demu sitaki umkose kabisa.
MIMI: Usijali kaka. Huyu mdogo mdogo mwisho wa siku utamkuta gheto kapumzika. Chezea Tandale wewe.
EDUADO: Hahaha!

AZIZA: Mambo!
MIMIl Mabaya.
AZIZA: Ubaya wake?
MIMI: Naumwa.
AZIZA: Nini tena jamani?
MIMI: Maralia. Yaani mbu mmoja tu jana chumbani kwangu ndio alisababisha majanga yote haya.
AZIZA: umekunywa dawa?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Kwa nini sasa jamani?
MIMI: Naogopa sana dawa Aziza. Labda uje uninyweshe kinguvu.
AZIZA: Dah! Pole sana Nyemo. Nitakuombea kwa Mungu akuponye.
MIMI: Asante sana. Nitafurahi sana.
AZIZA: Aya nishakushtua. Hebu niambie kuhusu vitu ulivyokuwa ukiniambia.
MIMI: Tatizo lako unajiamini sana Aziza halafu unafanya makosa sana kila unapoona kwamba fedha ndio kila kitu. Yaani haujifikirii kama kuna watoto wa matajiri ambao wanaumwa sana mpaka wanakufa, kama fedha ni kila kitu si wangepona.
AZIZA: Nafahamu.
MIMI: Basi kama unafahamu, fahamu pia kuna kitu ambacho ni kila kitu na si fedha kama unavyofikiria.
AZIZA: Kipi tena.
MIMI: Mungu ndiye kila kitu katika maisha yetu. Bila Mungu, huwezi kuwa na furaha hata kama una fedha, bila Mungu huwezi kupona ugonjwa wako hata kama una fedha na kutibiwa na madaktari wakubwa duniani. Umenipata?
AZIZA: Ndio nimekupata.
MIMI: Au hadi hapo unataka kubishana tena?
AZIZA: Hapana. Ila unaonekana kuwa na hekima sana Nyemo.
MIMI: Yeah! Unajua wakati mwingine yatupasa kuutambua ukweli. Hatutakiwi kuamini sana katika fedha. Ila achana na hayo. Wewe ni mama wa nyumbani, mwanafunzi wa sekondari au mwanafunzi wa chuo?
AZIZA: Naonekaje?
MIMI: Profile picha yako ni ya mdoli, sasa nitajua unaonekanaje?
AZIZA: Hahaha! Usijali. Mimi ni mwanachuo.
MIMI: Unasoma wapi?
AZIZA: Mlimani
MIMI: Unasomea nini?
AZIZA: Sheria.
MIMI: Afadhali.
AZIZA: Afadhali ya nini tena?
MIMI: Uje kuwa mwanasheria wangu baadae katika kampuni yangu.
AZIZA: Hahahah! Utaweza kunilipa?
MIMI: Kwa nini nisiweze? Nitakuwa na fedha mbayaaaaaaa....nitamiliki magari ya kifahari na majumba makubwa sana....lol
AZIZA: Yote ni mipango ya Mungu ila napenda ulivyoongea kwa sababu unaonekana una imani ya kupata hivyo, cha msingi yakupasa kujituma tu na kumtanguliza Allah kwa kila kitu. Naomba nikuulize swali.
MIMI: Usijali. Uliza.
AZIZA: Unaishi wapi?
MIMI: Tandale kwa Mtogole.
AZIZA: Kule kwenye wezi wengi na wakabaji?
MIMI: Si wezi wengi tu, kule kunapodharaulika na watu wenye fedha kama nyie.
AZIZA: Hahaha! Usiseme hivyo bwana. Ila mbona umedanganya?
MIMI: Nimedanganya nini?
AZIZA: Kwenye profile lako. Umeandika unaishi Romania. Ulikuwa unataka kujipaisha nini upate wanawake?
MIMI: Hapana Aziza. Hiyo imekuja yenyewe tu.
AZIZA: Kivipi?
MIMI: Nilikuwa nataka kupatambulisha kama home kwetu ni Tandale. Ila nilipokuwa nikiandika Tandale, haikuwa ikitambulika kama ilivyokuwa sehemu nyingine. Matokeo yao wao kama facebook wakaniletea Tandalesti mji fulani kutoka Romania, nikaona sio kesi, nikakubaliana nao, ila ukiangalia kwa makini, Tandale imetokeza katika jina hilo.
AZIZA: Yeah! Nimeona. Hebu naomba uniambie mengi kuhusu Tandale.
MIMI: Kama yapi unataka kufahamu?
AZIZA: Mazingira, watu wa huko na mambo mengine.
MIMI: Tandale kama Tandale mazingira yake mazuri sana, watu full kuyafurahia maisha kama kawa. Kuna watoto wazuri, watoto ambao wanajitambua wao ni nani na kipi cha kufanya maishani mwao. Kuna mambo ya Rusha Roho usiku, yaani kwa kifupi kuhusu maisha, huku tunakula sana bata kuliko kwenu pa kulala saa moja.
AZIZA: Hahaha! Kwani huko kwenu huwa mnalala saa ngapi?
MIMI: Huwa nikiwa mgonjwa sana, nawahi kulala kama saa saba hivi.
AZIZA: Saa saba?
MIMI: Yeah! Ila nikiwa si mgonjwa, mpaka adhana iadhiniwe. Watu tunatransform usiku kuwa mchana na maisha yanasonga.
AZIZA: U must be kidding me Nyemo.
MIMI: Huo ndio ukweli Aziza. Siwezi kukutania.

Unaona jinsi mawasiliano yetu yalivykuwa yakienda? Hapo ndipo nilipokuwa napataka sasa. Nilikuwa namletea sana ucheshi lakini mwisho wa siku kuna kitu nilikuwa nakihitaji kutoka kwake, namba ya simu tu. Unajua katika maisha ya kuchati facebook huwa yanachosha sana, kuna kipindi fulani automatically unatokea kummisi mtu fulani na ungependa sana awe online lakini hayupo online, unapokuwa na namba ya simu, inakupa wakati mzuri wa kumsikia na kumjulia hali katika kipindi chochote ambacho ungependa kumsikia.
Ucheshi ndio ulikuwa kawaida yangu ila katika kipindi hiki nilikuwa nataka kuuleta ucheshi mpaka katika maandishi. Aziza akaonekana kulifurahia hilo, akaonekana kuanza kunikubali japokuwa hatujawahi kuonana hata siku moja. Nilikuwa bize na chatting na Aziza, sikutaka kuwasiliana na mtu mwingine katika kipindi hicho japokuwa nilimuona Eduado, Ibra Akilimia na Emmanuel Solo walikuwa wamenitumia meseji.
Nilikuwa nikijitahidi sana kumuingiza Aziza kwenye himaya yangu, yaani aingie bila kupenda na mwisho wa siku kila kitu kiwe poa sana. Sikujali alikuwa akiishi wapi, sikujali na mimi nilikuwa nikiishi wapi, kitu ambacho nilikuwa nikikiamini ni kwamba mapenzi wala hayakuwa na hiyana, yalikuwa hayabagui watu kama tulivyo wanadamu.

AZIZA: Nikuulize kitu.
MIMI: Niulize tu.
AZIZA: Unasoma?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Unafanya kazi?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Sasa unafanya nini?
MIMI: Nipo nipo nyumbani. Nilisoma kidato cha kwanza, sikuwa na fedha za kuniendesha kielimu, nikaachana nayo mpaka sasa hivi. Kuna kipindi nilipata vijisenti mara baada ya kubeba sana mizigo Tandale sokoni, nikaenda kusoma English Course.
AZIZA: Kwa hiyo haufanyi kazi?
MIMI: Yeah! Sifanyi kazi.
AZIZA: Unafanya kitu gani kingine?
MIMI: Sifanyi chochote kile.
AZIZA: Ila niliona kama unaandika hadithi! Au majina yamefanana?
MIMI: Yeah! Huwa ninazipost tu.
AZIZA: Hadithi zile huwa unaandika wewe?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Sasa huwa anaandika nani?
MIMI: Anaandika baba na kisha mimi kuzichukua na kuziweka facebook.
AZIZA: Unanidanganya Nyemo.
MIMI: Nikudanganye ili iweje? Kuna tuzo ya uongo wanapewa waongo? Huo ndio ukweli.
AZIZA: Mmmh! Basi mpe hongera baba yako.
Mimi: Zimefika.

Wakati mwingine haitakiwi kuwa mkweli kwa kila kitu. Tayari nilikwishaona kwamba kagundua kwamba sisi ni watu tunaoishi sehemu mbili tofauti, madaraja mawili tofauti na katika kichwa chake aliamini kwamba Tandale wanaishi watu masikini japo haikuwa hivyo. Nilichokuwa nikikifanya ni kuendana na akili yake alivyokuwa ameiweka, nami nikaanza kujifanya masikini ambaye sikubahatika kusoma kwa kuwa sikuwa na fedha ya kuniendeleza kielimu. Nikafanikiwa, kwa kiasi fulani aina ya maisha ambayo nilimpa yalimfanya kuamini kwamba kweli nilikuwa mtoto wa uswahilini, nilijivunia kuishi Tandale katika uwepo wake.


ITAENDELEA  . . . 
  •  
    Support : Blog designer | Blogger | Developer | | KakyteeMedia.InC
    Copyright © 2011. Kakytee.com - All Rights Reserved
    Template Modified by KakyteeMedia
    Proudly powered by Blogger